Zaburi 112
Baraka Za Mwenye Haki 
 1 Msifuni Bwana. 
Heri mtu yule amchaye Bwana, 
mtu yule apendezwaye sana na amri zake. 
 2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, 
kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa. 
 3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, 
haki yake hudumu milele. 
 4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, 
yule mwenye rehema, huruma na haki. 
 5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, 
anayefanya mambo yake kwa haki. 
 6 Hakika hatatikisika kamwe, 
mtu mwenye haki atakumbukwa milele. 
 7 Hataogopa habari mbaya, 
moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana. 
 8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, 
mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake. 
 9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; 
haki yake hudumu milele; 
pembe yake itatukuzwa kwa heshima. 
 10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, 
atasaga meno yake na kutoweka, 
kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu. 
*^ Zaburi hii imetungwa kila mstari ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.